SUWASA YASHIRIKI MAADHIMISHO YA MEI MOSI KIMKOA SINGIDA
02-05-2026 10:40:12
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Singida (SUWASA) imeshiriki maadhimisho ya sikukuu ya wafanyakazi yaani Mei Mosi Iliyofanyika kimkoa katika uwanja wa Bombadia ambapo hii ni kuimarisha uhusiano na mshikamano thabiti baina ya wafanyakazi wake.Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, amewapongeza watumishi wote wakiwemo wa SUWASA kwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi na kuhakikisha wanamsaidia Rais katika kuwatumikia wananchi hali inayochangia kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.Katika tukio hilo, Mkuu wa Mkoa alipata fursa ya kuwatunukia vyeti watumishi hodari kutoka taasisi mbalimbali, wakiwemo watumishi wa SUWASA. Watumishi hao walitambuliwa kwa juhudi zao, nidhamu na utendaji bora kazini, hatua inayolenga kuhamasisha hari ya kazi na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa jamii.Aidha, jumla ya watumishi wanne (4) kutoka SUWASA wametunukiwa vyeti vya kutambua uhodari wao katika utendaji wa kazi ambapo Vyeti hivyo vimetolewa kama ishara ya kutumbua na kuthamini mchango wao katika taasisi.Akizungumza wakati wa utoaji wa vyeti, Halima Dendego aliwahimiza watumishi hao pamoja na wengine kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi na uwajibikaji ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za maji.Kaulimbiu ya maadhimisho hayo ilikuwa:“Kazi zenye staha ni nguzo imara kwa maendeleo endelevu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050.”